Powered by Blogger.

Advertise HERE!!

...

IDADI YA WALIOTEMBELEA

blog counter

Home Top Ad

Post Top Ad



Archive

Post Bottom Ad

AyoUpdates

AYOUPDATES | Thank you for choosing our website for viewing our latest news and posts. Please subscribe to our news letter to get our latest posts.

Home Ads

Breaking

ADMISSIONS

News

AFYA

Sports

NAFASI ZA KAZI

TECHNOLOGY&NEWS

Featured

Videos

Contact Form

Name

Email *

Message *

JIUNGE NASI KUPATA UPDATES ZA KAZI | HABARI ZA USAILI,ELIMU NA SCHOLARSHIPS


Sponsor

AD BANNER

Recent JOBS

About Me

authorHello, my name is Daniel Ngogo. I'm a blogger of this site.
Learn More →

Connect With us

Facebook

Popular Posts


MWONGOZO WA UTOAJI MIKOPO KWA 2019/2020

Bodi ya Mikopo ya WanafunzI wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2019/2020 ikiwa ni maandalizi ya kukaribisha maombi ya mikopo kwa mwaka ujao wa masomo wa 2019/2020.

Mwongozo huo wa kina unataja sifa za waombaji, utaratibu wa kuomba mikopo, na melekezo mengine muhimu, na unapatikana kwenye tovuti hii.

Kuupakua mwongozo

                       1. KWA KISWAHILI BOFYA HAPA.
                       2. IN ENGLISH CLICK HERE.

HESLB inatarajia kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2019/2020 kuanzia Juni 25, 2019 hadi Agosti 15, 2019, ikiwa imetenga kipindi cha majuma mawili kuwapa fursa waombaji wa mikopo watarajiwa kusoma kwa makini mwongozo huo na kujiandaa kuomba mikopo.

Aidha, HESLB inawakumbusha wanafunzi wanaotarajia kuomba mikopo ya shahada ya kwanza kuzingatia mambo yafuatayo:

Kuwa na nakala za vyeti vifuatavyo vilivyothibitishwa na Wakili, Hakimu
                             a). Cheti cha Kidato cha Nne;

                             b). Cheti cha Kidato cha Sita;

                             c). Cheti cha Stashahada (Diploma);

                             d). Cheti cha kuzaliwa

                             e). Cheti cha kifo cha mzazi au wazazi.

Nakala za vyeti (d na e) ziwe zimethibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar.

2. Aidha, Wanafunzi wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu huo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Kituo cha Afya cha Serikali;

3. Wanafunzi ambao walifadhiliwa masomo yao katika ngazi ya Sekondari au Stashahada (Diploma) wawe na barua za uthibitisho wa udhamini huo kutoka katika taasisi zilizogharamia masomo yao;

4. Waombaji wote wa mikopo wanakumbushwa kuusoma kwa makini mwongozo wa 2019/2020 na kuuzingatia.

Kwa maelezo zaidi, tuandikie kwa

Baruapepe: adcp@heslb.go.tz

logoblog